Thursday, September 27, 2018

KWANINI UNAHITAJI KUWA NA KAZI YAKO?



 

KUWA NA MTAZAMO CHANYA KATIKA MAISHA YAKO YA BAADAE (TAKE CONTROL OF YOUR FUTURE).

Ndugu tupo tupo kwenye mwendelezo wa kujifunza ni namna gani tunaweza kupiga hatua katika maisha yetu. Leo napenda tuangalie kwanini unahitaji kuwa na kazi yako?
Kuwa na mtazamo chanya katika maisha yako ya baadae (Take control of your future.) hebu tuangalie kwa kina kwanini unahitaji kuwa na kazi yako
1.UTARATIBU UMEBADILIKA (THE RULES HAVE CHANGED.)
           Tunaishi wakati wa shida sana . miaka michache iliyopita mfumo wa maisha ulikuwa tofauti kabisa na sasa hivi. Fikiria maisha ya karne ya 20 iliyopita ujaribu kulinganisha na leo. Asilimia kubwa ya watu wa leo wanasema uchumi umekuwa kati ya majanga makubwa katika maisha ya watu. Watu wengi wamekuwa wakiishi katika upande wa makali ya visu wengi wao wakiishi wakiwa hawana uhakika wa kesho watafanya nini?. Ni kweli natambua haya pengine unayajua  lakini unatambuaje kuhusu ni namna gani mtu anaweza kusimama hadi kufikia sehemu anayoitaka.Mtazamo chanya pekee ni suluhisho pekee katika kufikia ndoto zako.
2. NIMEKWAMBIA HIVYO (I TOLD  YOU SO).
           Umeshawahi kujiuliza na kutafakari ni kazi gani ambayo inaweza kuwa salama kwako? Sitaki kukatisha tamaa lakini Ukweli wa uhalisia ni kwamba hakuna kazi ambayo ipo salama siku zote. Lakini je unatafakari vipi kuhusu mtazamo wako katika maisha yako ya baadae. Unaweza kutupia lawama katika ngazi za juu n.k. lakini wewe kama wewe unasimamaje katika kutetea maendeleo yako.
3.HII NI KARNE MPYA (IT’S  A NEW CENTRUY ).
           Wakati nilipokuwa mtoto, wazazi wangu walinisihi njia sahihi ya kupata mafanikio ambayo ni ya uhakika ambayo nina imani hata wewe ulisihiwa ni kwamba:- Mwanangu nenda shule, kasome kwa bidii upate maksi nzuri ili uje upate kazi nzuri na ulipwe pesa kubwa na ili upate kazi kwa urahisi.
Lakini ndugu, napenda nikwambie hii ni karne mpya na  siyo tu karne mpya bali hadi mawazo ni mapya. Ndugu kazi  haiwezi kukuweka huru wala serikali haiwezi kukuweka huru bali mawazo yako ndio chombo pekee kitakachokuweka huru katika maisha yako yote..
4. MSTARI WA KIJANI AU MWEKUNDU.
Nimeita ni mstariwa kijani au mwekundu kwa sababu nikiangalia idadi ya watu waliopo ajirani kwenye mstari wa umaskini yazidi kupanda na idadi kubwa ya watu wanaofanya kazi zaidi ya umri wa miaka 60 yaongezeka. Na ninakuja napoteza maana halisi ya neno kustaafu maana sasa wazee wanapostaafu inakuwa kama ndio umefika muda wao wa kufanya kazi hakika nashindwa kuona mbele maana ni kiza tu lakini hapo hapo natambua ni kwa nini nahitaji kuwa na kazi yangu mapema .Tukiwa tunazidi kujifunza hebu naomba utafakari hayo na ninakuomba usikose hata makala moja zijazo karibu tena katika mwendelezo wa makala hii.

0 comments: