Friday, September 28, 2018

TIMIZA NDOTO ZAKO KWA KUFANYA MAMBO YAFUATAYO:-



Ndoto imekuwa ni kitendawili ambacho kimekuwa kikikosa jibu la moja kwa moja baina ya watu na kufanya wengi wao wakate tamaa katika safari yao ya kutimiza ndoto zao. Leo napenda kuzungumzia mambo yafuatayo yatakayokusaidia kupiga hatua katika mafanikio yako:-
1.    KUWA IMARA.
Mafanikio yetu yanategemea sana uimara wetu hasa katika upande wa afya zetu,ndugu kama itazolota na kulegea kweli upande wa kufikia malengo yako itakuwa ni kitendawili. Maana afya zetu zinapokuwa imara hapo tunaweza kukumbuka tufanye nini ili kufikia mahala Fulani tunapotaka kufika.
2.    FURAHIA MAISHA YAKO.
Ni kosa la jinai sana inapofikia hatua tunaanza kulaani maisha tuliyonayo , wengi tumekuwa tukilaani sana maisha tuliyonayo kwa sababu ya ugumu wake, changamoto zake n.k. lakini hatukumbuki kupitia hayo maisha tuliyonayo ni fursa pekee ambayo tunaweza kufanya vitu vikubwa ambavyo mwisho wa siku tutafurahia maisha yetu. Ndugu tunapofurahia maisha yetu inatupa chachu na hamasa zaidi katika kufight ndani ya maisha yetu na ndo kitu pekee kitakachomfanya mtu atomize ndoto zake haraka akiwa atafurahia nafasi aliyonayo na kuweza kufanya kazi kwa bidii zote.
3.    FANYA UTALII.
Neno utalii linakuja linatafasiriwa tofauti linapokuja kwenye mindset za watu kuwa hadi usafiri nje ya nchi ndo uwe umefanya utalii. Utalii upo wa aina nyingi ukiwa ni wa  nje au wa ndani na ya nchi. Ndugu unapokuwa unafanya utalii ni nafasi kubwa ya kuweza kujifunza mambo mengi yakiwemo biashara, kilimo, mazingira ya kuishi, uwekezaji n.k. maana unapokuwa unaishi mazingira yaleyale kila kukicha huingizi kitu chochote kichwani, yaani hujaona kitu kipya kwa muda mrefu kuna percentage kubwa sana ya akili kudumaa na kuona kumbe maisha ni hayahaya kwahiyo unapofanya utalii wa mazingira tofauti tofauti unafanya akili yako ifunguke kwa mambo mengi.
4.    TUNZA PESA.
Kati ya vitu ambavyo imekuwa ni mtihani mkubwa mzito ni namna gani ya kutunza pesa? Pesa imetawala kabisa fikira za watu na kushindwa ni namna gani ya kuikabili wanapoipata. Si rahisi sana kutambuia kama pesa inakutawala au laa lakini unapoweza kutunza pesa na kuweza kuifanyia vitu vya msingi ulivyoipangilia kabla hujaipata itakuwa ni rahisi sana kutimiza ndoto zako.
5.    SAIDIA WENGINE.
Kusaidia ni jambo jema ambalo linatakiwa lifanywe kwa kila mmoja wetu. Ndugu tunapokuwa na moyo wa kutoa na kusaidia wengine tunajijengea tabia ya kupokea na sisi na moyo wa utafutaji zaidi maana unapokuwa unatoa unajiandaa kupokea pia.
6.    TAFUTA KAZI MPYA.
Kazi unayofanya isiwe ni kikwazo cha kufikia ndoto zako wengi tumekuwa tukishindwa kuchukua maamuzi yaliyo sahihi hata kama mzigo umetuelemea  katika kazi zetu kwa kuhofia kushindwa kazi nyingine. Pale panapohitaji kuchukuliwa maamuzi yachukuliwe tu maana huwezi jua kilicho mbele yako kabla hujafika huko.


BADILI MATAZAMIO KUWA MALENGO

Imekuwa ni jambo la kawaida kila mwanzo wa kila mwaka watu kuwa na matazamio mbalimbali. Matazamio haya yamekuwa yakilenga hasa afya za watu, staili mbalimbali za maisha ikiwemo kupunguza uzito, kuacha kunywa pombe ,na kuvuta sigara, kupunguza matumizi ya pesa, na hata kufanya uwekezaji.
Lakini pamoja na hayo yote ,wiki chache tu zinapopita matazamio hayo husaulika hadi mwezi wa kumi na mbili unapokuja tena. Matazamio yamekuwa ni utangulizi wa kuweka alama kwa mwaka mpya tu. Katika makala hii hebu tujifunze na kluwa tofauti na ulenge hasa kwenye matazamio yako. Sasa ni namna gani unaenda kufanya matazamio yako kuwa malengo na klukufanya utimize ndoto zako.
Zifuatazo ni njia zitakazokufanya na kukusaidia uweze kufikia malengo yako ili utimize ndoto zako na siyo kubaki na ndoto zisizo timika.
1.     FANYA MATAZAMIO KUWA NDOTO ZAKO.
Watu wengi wamekuwa na utaratibu wa kuwa na matazamio na malengo halafu baada ya muda mfupi wanakata tamaa. Malengo yamekuwa na kufanywa ahadi za kawaida, ambazo zinakaa muda mfupi zinavunjika na kusahaulika. Ingawa kitendo cha kubadili matazamio hadi kuwa malengo ni kigumu sana na chenye kuhitaji kutumia akili nyingi hii yote ni kwa sababu Malengo na Ndoto ni kitu ambacho hupigania ili apate na kuondokana na shida alizonazo. Malengo ni kitu endelevu ambacho kinahitaji kukisimamia ili uweze kufikia ndoto zako.
2.     YAFANYE MATAZAMIO KUWA RAHISI.
Kosa la kwanza kabisa ambalo watu bwengi wanalifanya ni kuwa na malengo ambayo yanazidi maisha  yao na hii inapelekea kumfanya mtu aweze kukata tama haraka sana. Mabadiliko siku zote yanachukua muda na kutokana na hili mtu inakuwa ni vigumu sana kufikia malengo ambayo yanazidi kimo chake.
Kwamfano hauwezi ukawa na matazamio ya kuwa tajiri mkubwa duniani mwishoni mwa mwaka na wakati kwa sasa ni panya road. Na mvuta sigara vijiweni badala ya kuwa na mipangoya kuacha kuvuta sigara uanze mwanzo kama mtoto anayetembea kwa kuwa na matazamio kadri ya uwezo wako. Malengo yanapokuwa yamesetiwa makubwa kupita kiasi ni rahisi kufeli pindi mwili na akili zinapochukua muda mrefu kufanya kitu ambacho hakiwezekani . mabadiliko yanatakiwa kuwa taratibu na siyo harakaharaka.
3.     YAFANYE MATAZAMIO KUWA YA PEKEE.
Wakati unapopangilia mipango yako ya mwaka , ifanye mipango yako kuwa ya pekee. Upange mipango ambayo itakufanya ufikie mafanikio yako, mipango inayoainisha ndoto zako. Kama mtazamo wako ni kununua gari  sasa unatakiwa uainishe unataka kununua gari ya aina gani? Rangi yake na uweze kustick kwenye mipango yako ya kununua gari tu.
Watu mara nyingi huwa wana matazamio kwa mfanio aweze kupunguza uzito lakini anashindwa kuainisha kuainisha ni uzito wa kilo ngapi anatakiwa afikie . inakuwa ni vigumu sana kuona mabadiliko kitu ambachokitamfanya akate tamaa mapema.
4.     AINISHA MIPANGO YAKO.
Unaweza kuchora jedwali kwenye notebook la namna gani unaweza kufikia na kutimiza malengo yako. Kama malengo yako ni kutunza shillingi Millioni moja kwa mwaka sasa unatakiwa utengeneze bajeti ambayo kwa kila mwezi utakuwa unajaza kwenye jedwali lako na ukibainisha matumizi unayoyafanya. Au kwa mfano mtu ana mpango wa kuingia gym ni muhimu kubainisha ni gym gani unaenda kufanya, uitafute iko wapi, upange siku na muda sahihi wa kufanya gym.
5.     FURAHIA KIDOGO ULICHOPATA.
Watu hujifanya wagumu sana wanapokuwa pekee yao ukilinganisha wakiwa na watu wengine. Wanathubutu kujiadhibu wenyewe na kusababisha kushindwa kufikia malengo yao, maana unaposhindwa kutambua madogo uliyonayo utayatambuaje makubwa yale utakayoyapata?
Kusheherekea mafanikio hata kama yakiwa madogo ni muhimu sana kwa hatua ya mafanikio makubwa.
Kwa mfano unapokuwa na siku yako maalumu jaribu kuchukua muda hata wa lisaa limoja uweze kujipongeza mwenyewe kwa hatua uliyofikia  hata kama ni ndogo kiasi gani maana kupitia hicho kitu ulichokipata kitakupa hamasa na kukufanya uzidi kupiga hatua katika mafanikio yako.
6.     JIAMINI MWENYEWE.
Mwisho ,lakini muhimu sana ni jambo la kujiamini mwenyewe , hauwezi kufikia malengo yako kama  hauamini utayapata. Ni imani yako pekee itakayokufanya ufikie malengo yako. Inakuwa ni kitu cha ajabu mtu anapopanga kununua gari halafu hujiamini kama unaweza kununua,. Nguvu zote ambazo tunaanza nazo mwanzoni mwa mwaka tukijiamini na kwa ujasiri mkubwa hakika tutatimiza ndoto zetu.


Thursday, September 27, 2018

KWANINI UNAHITAJI KUWA NA KAZI YAKO?


 

KUWA NA MTAZAMO CHANYA KATIKA MAISHA YAKO YA BAADAE (TAKE CONTROL OF YOUR FUTURE).

Ndugu tupo tupo kwenye mwendelezo wa kujifunza ni namna gani tunaweza kupiga hatua katika maisha yetu. Leo napenda tuangalie kwanini unahitaji kuwa na kazi yako?
Kuwa na mtazamo chanya katika maisha yako ya baadae (Take control of your future.) hebu tuangalie kwa kina kwanini unahitaji kuwa na kazi yako
1.UTARATIBU UMEBADILIKA (THE RULES HAVE CHANGED.)
           Tunaishi wakati wa shida sana . miaka michache iliyopita mfumo wa maisha ulikuwa tofauti kabisa na sasa hivi. Fikiria maisha ya karne ya 20 iliyopita ujaribu kulinganisha na leo. Asilimia kubwa ya watu wa leo wanasema uchumi umekuwa kati ya majanga makubwa katika maisha ya watu. Watu wengi wamekuwa wakiishi katika upande wa makali ya visu wengi wao wakiishi wakiwa hawana uhakika wa kesho watafanya nini?. Ni kweli natambua haya pengine unayajua  lakini unatambuaje kuhusu ni namna gani mtu anaweza kusimama hadi kufikia sehemu anayoitaka.Mtazamo chanya pekee ni suluhisho pekee katika kufikia ndoto zako.
2. NIMEKWAMBIA HIVYO (I TOLD  YOU SO).
           Umeshawahi kujiuliza na kutafakari ni kazi gani ambayo inaweza kuwa salama kwako? Sitaki kukatisha tamaa lakini Ukweli wa uhalisia ni kwamba hakuna kazi ambayo ipo salama siku zote. Lakini je unatafakari vipi kuhusu mtazamo wako katika maisha yako ya baadae. Unaweza kutupia lawama katika ngazi za juu n.k. lakini wewe kama wewe unasimamaje katika kutetea maendeleo yako.
3.HII NI KARNE MPYA (IT’S  A NEW CENTRUY ).
           Wakati nilipokuwa mtoto, wazazi wangu walinisihi njia sahihi ya kupata mafanikio ambayo ni ya uhakika ambayo nina imani hata wewe ulisihiwa ni kwamba:- Mwanangu nenda shule, kasome kwa bidii upate maksi nzuri ili uje upate kazi nzuri na ulipwe pesa kubwa na ili upate kazi kwa urahisi.
Lakini ndugu, napenda nikwambie hii ni karne mpya na  siyo tu karne mpya bali hadi mawazo ni mapya. Ndugu kazi  haiwezi kukuweka huru wala serikali haiwezi kukuweka huru bali mawazo yako ndio chombo pekee kitakachokuweka huru katika maisha yako yote..
4. MSTARI WA KIJANI AU MWEKUNDU.
Nimeita ni mstariwa kijani au mwekundu kwa sababu nikiangalia idadi ya watu waliopo ajirani kwenye mstari wa umaskini yazidi kupanda na idadi kubwa ya watu wanaofanya kazi zaidi ya umri wa miaka 60 yaongezeka. Na ninakuja napoteza maana halisi ya neno kustaafu maana sasa wazee wanapostaafu inakuwa kama ndio umefika muda wao wa kufanya kazi hakika nashindwa kuona mbele maana ni kiza tu lakini hapo hapo natambua ni kwa nini nahitaji kuwa na kazi yangu mapema .Tukiwa tunazidi kujifunza hebu naomba utafakari hayo na ninakuomba usikose hata makala moja zijazo karibu tena katika mwendelezo wa makala hii.
UFANYE NINI UPIGE HATUA KATIKA MAISHA YAKO?








UTANGULIZI.

Uchumi upo kwenye hali mbaya (Tatters), Kazi yako ipo hatarini (trouble) na kama una kazi yako hujui ufanye nini?
Ni takribani dunia nzima imekubwa na janga hili la uchumi na mara nyingi bila hata kupata ufumbuzi wa moja kwa moja lakini pamoja na hayo yote si swala la kuhoji ni namna gani na kwasababu gani hayo yote yamekuwa yakitokea ,Swala la msingi ni kwamba ni kwa namna gani tunaweza kuzitumia hizo taarifa na kuzifanya upande wetu kuwa ni jambo jema la kujivunia na kuweza kuleta maendeleo upande wetu.
Nimekuwa nikijifunza biashara na kazi mbalimbali kutoka kwa watu tofauti tofauti , wakiwemo watu mashuhuri walioendelea na ambao hawajaendelea , wasomi (veryn educated) na ambao hawajasoma lakini kwa namna moja au nyingine hao wotewamekuwa wakihangaika hangaika na kubaki kulaumu kuwa uchumi umekuwa ni mgumu sana.
Huwa nafikiria sana kwanini inatokea mtu maskini na mtu tajiri ingali wanaweza wakawa sehemu moja na wakifanya kazi moja. Kipindi nipo shule nilisoma sana kwa bidii zote nikitarajia kuwa huru katika maisha haya na kuamini kuwa Elimu pekee ndio msingi wa Maendeleo lakini kadri nilivyokuwa nikizidi kusoma mambo yalikuwa tofauti na matarajio yangu. Sikatai kuwa Elimu siyo msingi wa Maendeleo  ila unaitumiaje Elimu yako katika maendeleo yako.
Nimesoma vitabu mbalimbali vikiongelea juu ya maswala haya ya uchumi na kupata mwangaza wa kutosha na namna gani tunaweza kupata uzoefu kuweza kukabiliana na changamoto za uchumi. Na leo napenda nikusihi vitu vifuatavyo vya msingi katika makala hii ya “Timiza Ndoto”.
1.Tafakari una chagua kutimiza ndoto zako ili mwisho wa siku uweze kuwa huru kiuchumi wako au kuwa Mtumishi katika maisha yako.
2.Tafakari  juu ya utawala wako wa kifedha ikiwa unaitawala au inakutawala.
Nimekuwa nikijiuliza ni namna gani mtu anawezaje kupata utajiri (Wealth) na akaweza na kuweza kubakia na utajiri katika maisha yake yote na asiwe mtumwa tena katika utafutaji na kuweza kustarehe kabisa.
Ndugu kupitia ukurasa huu wa blog ya “Timiza ndoto” tutajifunza tufanye nini katika karne hii ya 21 ili tuweze kupiga hatua katika maisha yetu .lakini kabla hatujaanza kuangalia kwa undani ni namna gani tunaweza kupiga hatua katika maisha yetu napenda nikusihi kitu kimoja cha msingi sana ambachio katika mihangaiko yako ya kila siku panga kuwa na kazi yako ambayo inaweza kukuweka huru katika kufanya mambo unayoyataka katika maisha yako.
Ahsante sana kwa muda wako uliotumia napenda nikukaribishe katika mwendelezo wa kujifunza ni namna gani tunaweza kupiga hatua katika maisha yetu.

Tuesday, September 25, 2018

KIJANA NA HAMASA: CHANGAMOTO YAKO NI IPI?

Ni siku nyingine tena ,kwa imani wewe ni mzima wa afya tele na ni tumaini langu hujambo kabisa.
Matatizo, Shida, Changamoto n.k Wengi wetu imekuwa ni sehemu ya maisha yetu, lakini je umewahi kujiuliza Changamoto yako ni ipi?
Changamoto zipo za kila aina zikiwemo changamoto za kiafya, Elimu, Uchumi kuyumba, Mila, Utamaduni n.k. Kwa leo napenda tutafakari juu ya changamoto ambayo imekuwa kilio kwa wengi wetu ambayo ni changamoto ya uchumi.
Ndugu katika makala zangu nimekuwa nikihusisha sana maswali siyo kwamba nataka nikusumbue ila nataka ujaribu kuumiza kichwa ,uwe mtu waku-reason yaani ushirikishe akili kutatua changamoto mbalimbali katika maisha yako. Changamoto ya Uchumi imekuwa ni kwa kila mtu si kwa maskini au matajiri lakini je umejaribu kufikiria ni sababu gani zinazosababisha iwe hivyo.
Katika siku ya leo napenda tutafakari sababu zifuatazo ambazo kwa upande wangu nahisi zimekuwa ni tatizo na chanzo kwa watu wengi kuyumba kwa uchumi.
Kwanza changamoto kubwa katika upande wa kujiinua kiuchumi ni Kutokujiamini kuthubutu (Wasiwasi) na Uzembe. Kitabu cha Retire young retire rich by Robert T. Kiyosaki aliandika“The biggest challenge you have is to challenge your own self-doubts and your laziness”Ndugu hebu jaribu kujitathimini upo kwenye dimbwi hili? Je ni fursa ngapi zimekupita ukiogopa kwamba wewe hauwezi na haustahili kufanya hivyo? Au ni kazi ngapi ambazo umekuwa mzembe wakufanya kwasababu za kusingizia mbalimbali. Robert T. Kiyosaki aliendelea kuandika “It is your self-doubts and your laziness that define and limit who you are” Kwa maana ya kwamba ni wasiwasi wako na uzembe wako unaokutambulisha na kukuonyesha kikomo chako jinsi gani ulivyo. Halafu akaendelea kusema “There is no one in your way except you and your doubts and If you will take on your self doubts and your laziness, you will find the door to your freedom”kwa maana ya kwamba “Hakuna njia yeyote tofauti na wewe na wasiwasi wako na kama utapata ufumbuzi wa wasiwasi wako na uzembe wako hakika utapata mlango wa uhuru wako.”
Note; Siku zote maamuzi sahihi ni yale anayoyachukua mtu bila kushirikishwa, kuna tofauti kubwa sana kati ya maamuzi na ushauri maana ushauri unaweza kuukubali au kuukataa lakini maamuzi yako ni msingi wa maisha yako.

Changamoto zipo nyingi sana na mtu sahihi wa kutatua changamoto yako ni wewe mwenyewe kikubwa ni kuamini unachokifanya kuwa ni sahihi. Naomba tukutane kwa makala nyingine tena katika makala zijazo katika mwendelezo wa makala zinazohusu kupata pesa na kuendelea kuwa na pesa na kutakia uwe na siku njema.