Sunday, March 11, 2018

KIJANA NA HAMASA: UKWELI KUHUSU NDOTO ZAKO


Ndoto ni kitu ambacho mtu hutamani kuwa na malengo ambayo kila mtu anawaza kufikia na kutimiza katika maisha yake. Japo kila mtu ana ndoto zake tofautitofauti, Changamoto inakuja kwenye kutimiza ndoto zake. Sio siri watu wamekuwa na ndoto ambazo siku zote hazitimii kwa sababu mbalimbali hadi kusababisha  kuwa na imani potofu na kujisema  Mungu hajampangia kufikia pale anapopahitaji kufika.Wapo watu wamekuwa na ndoto mbalimbali kama kuwa Profesa , Daktari ,Engineer, Mfanyabiashara n.k lakini mwisho wa siku anajikuta tofauti na alivyokuwa anawaza. Imekuwa changamoto kubwa inayosumbua watu wengi katika kutimiza ndoto. Mfano mzuri ni wewe hapo hivi kazi hiyo uliyonayo au kitu hicho unachofanya ndio zilikuwa ndoto zako tokea mwanzo?
Katika makala hii napenda nikushirikishe ni nini kwa sasa unaweza kufanya ili uweze kufanikisha ndoto zako. Naamini kama utafanya sawasawa na inavyotakiwa haitachukua muda kutimiza ndoto zako naomba uangalie kanuni ifuatayo ili uweze kutimiza ndoto zako.
MIPANGO +VITENDO ==>DARAJA==> NDOTO ZAKO
PLANS + ACTIONS==>BRIDGE ==>DREAMS
Najua una ndoto ambayo unayo na unatamani siku moja uitimize. Cha kufanya hebu kaa chini utafakari kwanza hiyo ndoto yako mfano una ndoto za kuwa mfanyabiashara mkubwa wa kitu Fulani .Kabla ya kufanya kitu chochote,
Kwanza Andaa Mpango mkakati unaohusu hiyo ndoto yako upangilie ni wapi uanzie na wapi uelekee na siri moja kubwa katika mipango yako ni kuwa na Imani na hicho unachokifanya naamini ukiseti mipango yako sawasawa itakuwa ni moja ya hatua katika kutimiza ndoto zako.
Pili ukishakamilisha mipango yako anza kufanyia Vitendo vile vyote unavyovipanga ukifuata hatua moja hadi hatua nyingine na kwa kufanya hivyo Mpango mkakati + na Vitendo itakuwa ni Daraja la Kutimiza Ndoto zako.
Ndugu, Tupo kwenye dunia iliyojaa maarifa ya kila aina na kila kukicha vitu vipya vinabuniwa  ili kusaidia watu kufanya mambo yao kwa urahisi na kwa muda husika ni wakati wako sasa kufikiria ufanye nini ili uweze kwenda jinsi dunia inavyokwenda.kwa maelezo zaidi juu ya chochote unachoweza au unatamani ufanye unaweza kunitafuta kupitia whatsap no.iliyopo hapo chini. Ahsante sana kwa muda tukutane tena katika makala zijazo kwa kutambua na kuelewa maarifa zaidi.

1 comment: