Saturday, October 13, 2018

USIKUBALI KUSHINDWA.




Kufeli katika mipango au mikakati uliyojiwekea ni kitu ambacho kinatokea kwa kila mtu. Na ni wakati ambao mtu anakuwa njia panda katika kufanya maamuzi ama kuendelea au kuacha.
Wakati unapopitia hatua hii katika mipango yako huu sio wakati wa kuruhusu na kukufanya wewe uweze kukata tamaa katika safari yako badala yake unatakiwa upanue ufahamu wako ujue ni namna gani ya kuendelea na kukufanya ufike pale ulipotaka kufika.
Ndugu napenda kukuambia kitu cha msingi sana ambacho unatakiwa kukifanya endapo utaanza kuona dalili za kufeli katika mipango yako, kwanza unatakiwa ujue kwamba hutakiwi kujiona kama wewe ni mkamilifu kwa kitu ambacho unakifanya (do not need to be perfect or perfectly extraordinary just be better version of you

Mara nyingi tumekuwa tukiangalia hasa mabadiliko ya vitu tunavyovifanya tukisahau kuangalia mipangilio yetu ikoje na inaendeleaje? Kufanya kazi kwa muda mrefu bila kuona mabadiliko hakumanishi kama mipango yako imekufa au laa , hapo kinachotakiwa na kusubiriwa ni wewe kujua unatakiwa upangilie kwa namna gani ili uweze kuona mabadiliko unayoyataka. Mwandishi mmoja aliandika  “When you have a day when you fall down on the diet, instead of telling yourself that you are weak or bad, tell yourself that you had a bad day and that tommorrow’s a new day to start is over.”

Ni muhimu sana kuwa mstahimilivu , kuwa na upeo wa kutambua kitu mapema itakusaidia sana kusonga mbele katika safari yako halafu tambua ni rahisi sana kukata tamaa kuliko kujipa moyo hivyo badala ya kuruhusu mawazo hasi yanayokujia kwenye ufahamu wako ni muda sasa wa kuwa na mawazo chanya na kuondoa yote mawazo mawazo ambayo yatakupelekea kukata tamaa katika kufikia ndoto zako.

0 comments: