Sunday, October 21, 2018




Hakika penye nia pana njia , ni tumaini langu tumekuwa tukinufaika sana na mafundisho haya ya Timiza ndoto napenda kukukaribisha sana wewe msomaji kama ni mara ya kwanza basi tumekuwa na makala mbalimbali ambazo zimekuwa zikifafanua kwa undani na jinsi gani tunaweza kufanya ili kuweza kufikia ndoto zetu ambazo zimekuwa ni kitendawili kisichokuwa na jibu katika maisha yetu haya. Naomba twende pamoja katika makala ya leo ya UMEJITOA? 

Ili ufanikiwe kwa kiwango kikubwa sana ni muhimu sana kujitoa katika maisha yako. Kwa leo napenda nizungumzie hili neno kujitoa kwa namna nyingine kidogo. Watu tumekuwa tukipambana na kuwa na jitihada kubwa sana katika maisha yetu lakini bado kuna vitu tumekuwa tukivishikilia ambavyo kwa namna moja au nyingine vimekuwa ni kikwazo katika kufikia ndoto zetu. Ninaposema kujitoa naamanisha ni muhimu uache kufanya vitu Fulani ambavyo unavipenda sana kuvifanya ila vinakurudisha nyuma ama havina mchango wowote katika maendeleo yako.
Kuna vitu vingi sana ambavyo unapenda kuvifanya na unavifurahia. Ila kwa kuendelea kufanya vitu hivyo inakuwa ni vigumu sana kwako kuwa tajiri. Ni muhimu ujue vitu hivyo na kuviacha mara moja ili uweze kufanya vile vitakavyokufikisha kwenye ndoto zako. Kwa mfano kama unapenda kutumia fedha kwenye starehe kwa kiwango kikubwa inakubidi upunguze sana au uache kabisa starehe hizo ili utumie fedha zako vizuri kuwekeza na utumie muda uliokuwa unaupoteza kwenye starehe kujifunza zaidi kuhusu kazi au biashara zako. Unaweza fikiri kuacha starehe ni jambo la kawaida tu  ni lazima ujitoe maana kama kitu umekizoea  ni vigumu sana kusema  kuanzia sasa unaachana nacho na ukaacha kweli.

NI NAMNA GANI TUNAWEZA KUJITOA?
Ili uweze kufikia ndoto zako kweli ni lazima ujitoe. Kuna vitu ambavyo inabidi uache kuvifanya au kujihusisha navyo mara moja ili uweze kupata muda zaidi wa kufikiria malengo na ndoto zako.
Najua mpaka sasa umeshaweka malengo na mipango itakayokufikisha kwenye ndoto zako na pia umeshapanga matumizi mazuri ya muda wako pengine tayari umeshaandika vitu vyote unavyotamani kuwa navyo kwa baadae sasa ili kujitoa naomba ufanye hivi;
Chukua kalamu na karatasi ama notebook na uandike vitu vyote unavyofanya na muda wako kuanzia muda unaoamka mpaka muda unaorudi kulala ukijumlisha na muda wa kulala. Fikiria kwa wiki chache zilizopita vitu ambavyo umekuwa unafanya kila siku. Baasa ya kuandika vitu hivyo angalia ni vitu gani vinachukua muda wako mwingi na umuhimu wake kwenye malengo ya kutimiza ndoto zako. Kama vitu hivyo havina mchango kwenye malengo yako viache mara moja. Vitu kama kwenda baa kila siku, kuangalia tv zaidi ya masaa mawili kwa siku, kupiga hadithi zisizo na msaada kwako na mabishano yasiyo ya msingi unatakiwa uviache mara moja. Kama unalala zaidi ya masaa nane pia unapoteza muda hivyo punguza muda wa kulala uwe nane au saba kwa siku.
Chukua kalamu na karatasi tena na uandike vitu vyote ambavyo vinatumia fedha zako. Andika vitu vyote ambavyo vinatumia fedha zako. Andika vitu vyote ambavyo unanunua kila siku, wiki na hata mwezi. Kisha angalia ni vitu gani ambavyo sio muhimu sana kwenye malengo yako na maisha yako uvitoe kabisa. Matumizi yote ya fedha ambayo ni ya anasa unaweza kuyatoa kwa sasa unapotengeneza njia za kutimiza ndoto zako.
Kitu chochote ambacho unapenda sana kukifanya ila hakina msaada wowote kwako kufikia malengo ya kuwa tajiri inabidi uache kuvifanya mara moja ili uanze kufanya vile vitakavyokufikisha kwenye ndoto zako.
Ahsante sana kwa siku ya leo napenda nikukaribishe katika makala nyingine inayofuata ikielezea kwa undani MTAZAMO WAKO NI UPI KUHUSU MAISHA YAKO. 

0 comments: