Hakika penye nia pana
njia , ni tumaini langu tumekuwa tukinufaika sana na mafundisho haya ya
Timiza ndoto napenda kukukaribisha sana wewe msomaji kama ni mara ya kwanza
basi tumekuwa na makala mbalimbali ambazo zimekuwa zikifafanua kwa undani na
jinsi gani tunaweza kufanya ili kuweza kufikia ndoto zetu ambazo zimekuwa ni
kitendawili kisichokuwa na jibu katika maisha yetu haya. Naomba twende pamoja
katika makala ya leo ya UMEJITOA?
Ili
ufanikiwe kwa kiwango kikubwa sana ni muhimu sana kujitoa katika maisha yako.
Kwa leo napenda nizungumzie hili neno kujitoa kwa namna nyingine kidogo. Watu
tumekuwa tukipambana na kuwa na jitihada kubwa sana katika maisha yetu lakini
bado kuna vitu tumekuwa tukivishikilia ambavyo kwa namna moja au nyingine
vimekuwa ni kikwazo katika kufikia ndoto zetu. Ninaposema kujitoa naamanisha ni
muhimu uache kufanya vitu Fulani ambavyo unavipenda sana kuvifanya ila
vinakurudisha nyuma ama havina mchango wowote katika maendeleo yako.
Kuna vitu
vingi sana ambavyo unapenda kuvifanya na unavifurahia. Ila kwa kuendelea
kufanya vitu hivyo inakuwa ni vigumu sana kwako kuwa tajiri. Ni muhimu ujue
vitu hivyo na kuviacha mara moja ili uweze kufanya vile vitakavyokufikisha
kwenye ndoto zako. Kwa mfano kama unapenda kutumia fedha kwenye starehe kwa
kiwango kikubwa inakubidi upunguze sana au uache kabisa starehe hizo ili utumie
fedha zako vizuri kuwekeza na utumie muda uliokuwa unaupoteza kwenye starehe
kujifunza zaidi kuhusu kazi au biashara zako. Unaweza fikiri kuacha starehe ni
jambo la kawaida tu ni lazima ujitoe
maana kama kitu umekizoea ni vigumu sana
kusema kuanzia sasa unaachana nacho na
ukaacha kweli.
NI NAMNA
GANI TUNAWEZA KUJITOA?
Ili uweze
kufikia ndoto zako kweli ni lazima ujitoe. Kuna vitu ambavyo inabidi uache
kuvifanya au kujihusisha navyo mara moja ili uweze kupata muda zaidi wa
kufikiria malengo na ndoto zako.
Najua mpaka
sasa umeshaweka malengo na mipango itakayokufikisha kwenye ndoto zako na pia
umeshapanga matumizi mazuri ya muda wako pengine tayari umeshaandika vitu vyote
unavyotamani kuwa navyo kwa baadae sasa ili kujitoa naomba ufanye hivi;
Chukua
kalamu na karatasi ama notebook na uandike vitu vyote unavyofanya na muda wako
kuanzia muda unaoamka mpaka muda unaorudi kulala ukijumlisha na muda wa kulala.
Fikiria kwa wiki chache zilizopita vitu ambavyo umekuwa unafanya kila siku.
Baasa ya kuandika vitu hivyo angalia ni vitu gani vinachukua muda wako mwingi
na umuhimu wake kwenye malengo ya kutimiza ndoto zako. Kama vitu hivyo havina
mchango kwenye malengo yako viache mara moja. Vitu kama kwenda baa kila siku,
kuangalia tv zaidi ya masaa mawili kwa siku, kupiga hadithi zisizo na msaada
kwako na mabishano yasiyo ya msingi unatakiwa uviache mara moja. Kama unalala
zaidi ya masaa nane pia unapoteza muda hivyo punguza muda wa kulala uwe nane au
saba kwa siku.
Chukua
kalamu na karatasi tena na uandike vitu vyote ambavyo vinatumia fedha zako.
Andika vitu vyote ambavyo vinatumia fedha zako. Andika vitu vyote ambavyo
unanunua kila siku, wiki na hata mwezi. Kisha angalia ni vitu gani ambavyo sio
muhimu sana kwenye malengo yako na maisha yako uvitoe kabisa. Matumizi yote ya
fedha ambayo ni ya anasa unaweza kuyatoa kwa sasa unapotengeneza njia za
kutimiza ndoto zako.
Kitu
chochote ambacho unapenda sana kukifanya ila hakina msaada wowote kwako kufikia
malengo ya kuwa tajiri inabidi uache kuvifanya mara moja ili uanze kufanya vile
vitakavyokufikisha kwenye ndoto zako.
Ahsante sana
kwa siku ya leo napenda nikukaribishe katika makala nyingine inayofuata
ikielezea kwa undani MTAZAMO WAKO NI UPI KUHUSU
MAISHA YAKO.


