Friday, March 9, 2018

KIJANA NA HAMASA: WOGA NYUMBA YA UMASKINI.





Kilio ,Ni kilio kila kukicha afadhali ya jana. Limekuwa ni janga kati ya majanga yanayosumbua barani Afrika yakiwemo Vita , Maradhi n.k
 Umaskini umekuwa ni tatizo la kukaliwa kila leo kutafuta ufumbuzi ni namna gani wanaweza kuondokana na janga hili. Wasomi mbalimbali wameumiza vichwa ni jinsi gani wanaweza kuondokana na janga hili na sio wasomi tu ni tatizo ambalo limekuwa kwa kila mtu aweze kujinusuru na umaskini.
Katika siku ya leo napenda tuangalie hasa kwa undani maana ya umaskini na sababu zinazofanya mtu awe maskini kila kukicha.
Umaskini ni nini?
Kwa tafasri ya harakaharaka Umaskini ni hali ile kitu au mtu anaposhindwa kukidhi na kumudu mahitaji yake kwa muda sitahiki.
Ni maswali mengi unaweza kujiuliza “Je Umaskini ni kukoswa pesa?” au “Je pesa ndio suluhisho la umaskini?” Katika maswali haya unaweza ukawa na majibu ya moja kwa moja kwamba jibu sahihi ni Pesa lakini hebu jaribu kufikiri tena “Je hauwezi kuwa na Pesa na bado ukaendelea kuwa maskini?” Mpendwa msomaji najaribu kukuweka kwenye ulimwengu wa Fikra ujaribu kupambanua wewe kama wewe halafu katika hayo maswali sidhani kama utakoswa jibu.
Kabla sijaenda kuelezea sababu zinazofanya mtu au nchi ikiwemo Tanzania kuendelea kuwa maskini napenda kukuweka wazi kuhusu swala la umaskini. Sio siri kwa mienendo yetu na tabia zetu za kutotambua tunafanya nini na kugandisha  akili zetu zisitake kupanuka na kutaka kila kitu mtelezo waswahili wanavyosema ganda la ndizi tutaendelea kuwa maskini siku hadi siku.
Umaskini sio swala la kukoswa pesa au kuwa na pesa kidogo bali umaskini unaletwa na jinsi gani akili zetu tulivyozilaza hatutaki kushirikisha katika maendeleo maana hata wewe ni shahidi katika umri huo ulio nao sizani kama huna historia ya mtu kumiliki pesa halafu akafirisika na kuishiwa kila kitu hapohapo unaweza kujiuliza ni sababu gani zinamfanya mtu awe na maendeleo halafu ifikie hatua  aishiwe kila kitu. Kumbe tukiangalia uhalisia Umaskini hausababishwi na ukosefu wa pesa ila ni uwezo wa kufikiri na nidhamu katika maendeleo ya mtu Mfano mzuri Mtu anakuwa ana uwezo wa kipato cha laki mbili kwa mwezi lakini nyumba anayoishi amepanga kwa elfu themanini bado anategemea aende shopping  isiyopungua elfu hamsini hapohapo hicho kipato kimulishe na bado hajamtumia mama unafikiri mtu kama huyo baada ya miaka miwili atakuwa na maendeleo gani?
Sababu za Umaskini.
Ndugu, kuna sababu nyingi sana ambazo tunaweza kuziona zinasababisha umaskini ikiwemo vita, ufisadi, maradhi, uvivu na Uzembe, Ukosefu wa Elimu na mambo mengi kadha wa kadha.
Hizo ni baadhi ya sababu zinazochukuliwa kwa tathmini ya umaskini katika nchi n.k “Je unaweza kufikiria sababu hizo ni ukweli zinachangia umaskini hadi kwa mtu binafsi?” jibu najua utakuwa nayo Hebu sasa tuangalie ni sababu nne ambazo mara nyingi zinachangia sana Ongezeko la umaskini barani afrika na hasa kwa wananchi wengi wa Tanzania.
Kwanza “Woga” ni ugonjwa wa maendeleo ambao unahitaji maamuzi yaliyo sahihi kwa mtu binafsi kuweza kujitibu ndugu, sidhani neno  woga linaweza kuwa msamiati kwa mtu anayejua kusoma na kuandika lakini ni ugonjwa mbaya mno katika maendeleo ya mtu na taifa kwa ujumla maana inapofika mahali pa kuchukua maamuzi yaliyo sahihi mtu anaogopa na hili lipo kwa watanzania wengi sana Mfano rahisi ni mtu anapotaka labda kufungua biashara kitu cha kwanza anachowaza ni kwamba  nikipata hasara itakuwaje baada ya kuwaza afungue biashara aboreshe kiasi gani ilia pate soko anawaza kushindwa na kupata hasara na hii imekuwa inarudisha watu nyuma sana na kuendelea kuwa maskini. Ndugu yangu kama una tatizo kama hili nafasi bado unayo chukua maamuzi yaliyo sahihi kwa kile unachofikiria kinaweza kukufanya ufikie ndoto zako ufanye kwa imani yako yote utafanikiwa.
Pili “Ukosefu wa Elimu bora ” Watanzania walio wengi wanashindwa kuendelea sababu ya ukosefu wa Elimu bora ya kujikimu na kuendesha mipango yao madhubuti .Hii pia inaweza kusababishwa na mfumo wa elimu yetu nchini maana sio siri msomaji Mtanzania anaweza kusoma hadi chuo kikuu halafu akaletwa mtaani akaambiwa afanye chochote alichosomea ili kimusaidie katika maisha yake bila kupatiwa ajira (ajiajiri mwenyewe) hawezi.Je unaweza kufikiri tunaelekea wapi? Lakini si hivyo tu kuna kundi kubwa sana ambalo hawawezi hata kujisamamia hata kidogo sababu ya ukosefu wa elimu bora.
Tatu “Uvivu na Uzembe” ni moja ya sababu ambayo inakumba kundi kubwa la watu hasa nchini kwetu ambapo watu wanashindwa kujishughulisha hata kwa kipato kidogo kuweza kujipatia riziki hivyo mtu anabaki na maisha duni na kubaki tegemezi  na maskini kila kukicha.
Nne na Muhimu “Nidhamu ya Pesa” hakuna kitu kinachorudisha na kufanya mtu kuwa na maisha duni na kubaki maskini ni ukosefu wa nidhamu ya pesa mfano mtu yupo tayari kuwa na matumizi ambayo yanazidi kipato  kwa makala zijazo nitaelezea kwa undani ni namna gani mtu anaweza kuwa na nidhamu ya pesa na ikamsaidia katika mafanikio yake na kufikia ndoto zake.


1 comment:

  1. hakika maamuzi yaliyo sahihi ni yale anayochukua mtu bila kushirikishwa

    ReplyDelete