Kilio ,Ni kilio kila kukicha afadhali ya jana. Limekuwa ni
janga kati ya majanga yanayosumbua barani Afrika yakiwemo Vita , Maradhi n.k
Umaskini umekuwa ni
tatizo la kukaliwa kila leo kutafuta ufumbuzi ni namna gani wanaweza kuondokana
na janga hili. Wasomi mbalimbali wameumiza vichwa ni jinsi gani wanaweza
kuondokana na janga hili na sio wasomi tu ni tatizo ambalo limekuwa kwa kila
mtu aweze kujinusuru na umaskini.
Katika siku ya leo napenda tuangalie hasa kwa undani maana
ya umaskini na sababu zinazofanya mtu awe maskini kila kukicha.
Umaskini ni nini?
Kwa tafasri ya harakaharaka Umaskini ni hali ile kitu au mtu
anaposhindwa kukidhi na kumudu mahitaji yake kwa muda sitahiki.
Ni maswali mengi unaweza kujiuliza “Je Umaskini ni kukoswa
pesa?” au “Je pesa ndio suluhisho la umaskini?” Katika maswali haya
unaweza ukawa na majibu ya moja kwa moja kwamba jibu sahihi ni Pesa lakini hebu
jaribu kufikiri tena “Je hauwezi kuwa na Pesa na bado
ukaendelea kuwa maskini?” Mpendwa msomaji najaribu kukuweka kwenye
ulimwengu wa Fikra ujaribu kupambanua wewe kama wewe halafu katika hayo maswali
sidhani kama utakoswa jibu.
Kabla sijaenda kuelezea sababu zinazofanya mtu au nchi
ikiwemo Tanzania kuendelea kuwa maskini napenda kukuweka wazi kuhusu swala
la umaskini. Sio siri kwa mienendo yetu na tabia zetu za kutotambua tunafanya
nini na kugandisha akili zetu zisitake
kupanuka na kutaka kila kitu mtelezo waswahili wanavyosema ganda la ndizi
tutaendelea kuwa maskini siku hadi siku.
Umaskini sio swala la kukoswa pesa au kuwa na pesa kidogo
bali umaskini unaletwa na jinsi gani akili zetu tulivyozilaza hatutaki
kushirikisha katika maendeleo maana hata wewe ni shahidi katika umri huo ulio
nao sizani kama huna historia ya mtu kumiliki pesa halafu akafirisika na
kuishiwa kila kitu hapohapo unaweza kujiuliza ni sababu gani zinamfanya mtu awe
na maendeleo halafu ifikie hatua aishiwe
kila kitu. Kumbe tukiangalia uhalisia Umaskini hausababishwi na ukosefu wa pesa
ila ni uwezo wa kufikiri na nidhamu katika maendeleo ya mtu Mfano mzuri Mtu
anakuwa ana uwezo wa kipato cha laki mbili kwa mwezi lakini nyumba anayoishi
amepanga kwa elfu themanini bado anategemea aende shopping isiyopungua elfu hamsini hapohapo hicho kipato
kimulishe na bado hajamtumia mama unafikiri mtu kama huyo baada ya miaka miwili
atakuwa na maendeleo gani?
Sababu za Umaskini.
Ndugu, kuna sababu nyingi sana ambazo tunaweza kuziona
zinasababisha umaskini ikiwemo vita, ufisadi, maradhi, uvivu na Uzembe, Ukosefu
wa Elimu na mambo mengi kadha wa kadha.
Hizo ni baadhi ya sababu zinazochukuliwa kwa tathmini ya
umaskini katika nchi n.k “Je unaweza kufikiria sababu hizo ni
ukweli zinachangia umaskini hadi kwa mtu binafsi?” jibu najua
utakuwa nayo Hebu sasa tuangalie ni sababu nne ambazo mara nyingi zinachangia
sana Ongezeko la umaskini barani afrika na hasa kwa wananchi wengi wa Tanzania.
Kwanza “Woga” ni ugonjwa wa
maendeleo ambao unahitaji maamuzi yaliyo sahihi kwa mtu binafsi kuweza kujitibu
ndugu, sidhani neno woga linaweza kuwa
msamiati kwa mtu anayejua kusoma na kuandika lakini ni ugonjwa mbaya mno katika
maendeleo ya mtu na taifa kwa ujumla maana inapofika mahali pa kuchukua maamuzi
yaliyo sahihi mtu anaogopa na hili lipo kwa watanzania wengi sana Mfano rahisi
ni mtu anapotaka labda kufungua biashara kitu cha kwanza anachowaza ni
kwamba nikipata hasara itakuwaje baada
ya kuwaza afungue biashara aboreshe kiasi gani ilia pate soko anawaza kushindwa
na kupata hasara na hii imekuwa inarudisha watu nyuma sana na kuendelea kuwa
maskini. Ndugu yangu kama una tatizo kama hili nafasi bado unayo chukua maamuzi
yaliyo sahihi kwa kile unachofikiria kinaweza kukufanya ufikie ndoto zako
ufanye kwa imani yako yote utafanikiwa.Pili “Ukosefu wa Elimu bora ” Watanzania walio wengi wanashindwa kuendelea sababu ya ukosefu wa Elimu bora ya kujikimu na kuendesha mipango yao madhubuti .Hii pia inaweza kusababishwa na mfumo wa elimu yetu nchini maana sio siri msomaji Mtanzania anaweza kusoma hadi chuo kikuu halafu akaletwa mtaani akaambiwa afanye chochote alichosomea ili kimusaidie katika maisha yake bila kupatiwa ajira (ajiajiri mwenyewe) hawezi.Je unaweza kufikiri tunaelekea wapi? Lakini si hivyo tu kuna kundi kubwa sana ambalo hawawezi hata kujisamamia hata kidogo sababu ya ukosefu wa elimu bora.
Tatu “Uvivu na Uzembe” ni moja
ya sababu ambayo inakumba kundi kubwa la watu hasa nchini kwetu ambapo watu
wanashindwa kujishughulisha hata kwa kipato kidogo kuweza kujipatia riziki
hivyo mtu anabaki na maisha duni na kubaki tegemezi na maskini kila kukicha.
Nne na Muhimu “Nidhamu ya Pesa” hakuna
kitu kinachorudisha na kufanya mtu kuwa na maisha duni na kubaki maskini ni
ukosefu wa nidhamu ya pesa mfano mtu yupo tayari kuwa na matumizi ambayo yanazidi
kipato kwa makala zijazo nitaelezea kwa
undani ni namna gani mtu anaweza kuwa na nidhamu ya pesa na ikamsaidia katika
mafanikio yake na kufikia ndoto zake.

hakika maamuzi yaliyo sahihi ni yale anayochukua mtu bila kushirikishwa
ReplyDelete