Ndugu, Tupo kwenye dunia iliyojaa maarifa ya kila aina na
kila kukicha vitu vipya vinabuniwa ili
kusaidia watu kufanya mambo yao kwa urahisi na kwa muda husika ni wakati wako
sasa kufikiria ufanye nini ili uweze kwenda jinsi dunia inavyokwenda.
Maarifa ni njia inayotumiwa kujitoa katika shida.Maarifa ni
njia ya kupata kitu.Maarifa ni Elimu au ujuzi ambao anaupata mtu ili uweze kumsaidia kutatua
changamoto mbalimbali zinazojitokeza.
Watu wengi wanatafuta elimu ili iwasaidie kupata kazi; hayo
ni makosa makubwa. Unachopaswa kutafuta ni MAARIFA ili yakusaidie kupata kazi
ya kufanya.
Wengi husema Pesa ni kila kitu katika dunia hii. Sio kweli
lakini naweza kusema Pesa ina nafasi kubwa sana katika dunia lakini cha muhimu katika
vyote hivyo ni MAARIFA maana naamini ukiwa
na maarifa unaweza kuwa na chochote unachokitaka. Katika siku ya leo napenda
tuangalie ni nini hasa nguvu ya maarifa na inakusaidiaje katika mambo yako.
VITABU ni
nguvu kubwa sana ya maarifa ambayo inafanya watu wazidi kuwa wabunifu kila
kukicha lakini changamoto kubwa ipo kwa Waafrika maana hadi siku umekuwepo
msemo unaosema Ukitaka umfiche Mwaafrika kitu cha thamani Kiandike kwenye
Kitabu
Mpendwa leo napenda kukuhamasisha tu ya kwamba ukitaka
kufanikiwa na kuendelea kwa kasi ya 4g ni kusoma Vitabu maana katika vitabu
unaweza kujizolea faida nyingi sana kama ifuatavyo;
Ubunifu watu wengi sana
wamekuwa wabunifu na kuzidi kugundua mambo mapya sababu ya kusoma vitabu
ambavyo vinawafanya kuwa welevu na kupata maarifa mbalimbali ambayo
wanapoyatumia katika hisia chanya yanawaletea maendeleo makubwa sana katika
maisha yao na jamii inayowazunguka.
Uhamasikaji ,Tupo kwenye
dunia ambayo imejaa vikwazo na vigingi vingi sana watu wamekuwa wakikatishana tamaa
sababu ya kukoswa maarifa ndugu ukiwa una nasoma vitabu utahamasika na kupata
nguvu ya kufanya mambo makubwa ambayo hata ulikuwa hutarajii kufanya katika
maisha yako.
Kutunza muda wako ndugu
naamini unapokuwa unatenga muda wa kusoma vitabu itakufanya kuwa makini na muda
wako na kujijengea tabia ya
kujisomea, moja kwa moja unaanza kujijengea tabia ya kutunza muda. Hutapoteza
tu muda na kuona huna cha kufanya kwa sababu muda wote una kitabu cha kusoma.
Na pale ambapo una kitu cha kukusukuma umalize kitabu haraka kila dakika chache
utakazopata utazitumia vizuri kusoma
Kuongeza Kipato chako
Unapokuwa msomaji wa vitabu naamini utakuwa mbunifu , utahamasika ,utaweza
kutunza muda wako kitu ambacho kitakuwezesha kuongeza kipato chako katika kitu
chochote unachokifanya
Kuna faida nyingi sana unaweza kupata kupitia kusoma vitabu
ndugu kama hujaanza au huna pa kuanzia naomba unitafute kwa namba na email
iliyopo hapo chini niweze kukupa mwanga zaidi ni nini ufanye ili tuweze kwenda
sawasawa na dunia yetu hii iliyojaa maarifa na ubunifu wa kila kukicha sio
mwingine ni mimi muhamasishaji wako Yohana Shigukulu ahsante sana kwa muda wako
kuutumia na kuweza kusoma makala hii naomba tukutane kwa makala zijazo.

Moja ya silaha kubwa katika mafanikio ni kujua maarifa
ReplyDelete