Monday, March 12, 2018

KIJANA NA HAMASA: NGUVU YA MAARIFA


Ndugu, Tupo kwenye dunia iliyojaa maarifa ya kila aina na kila kukicha vitu vipya vinabuniwa  ili kusaidia watu kufanya mambo yao kwa urahisi na kwa muda husika ni wakati wako sasa kufikiria ufanye nini ili uweze kwenda jinsi dunia inavyokwenda.
Maarifa ni njia inayotumiwa kujitoa katika shida.Maarifa ni njia ya kupata kitu.Maarifa ni Elimu au ujuzi ambao anaupata mtu ili uweze kumsaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza.
Watu wengi wanatafuta elimu ili iwasaidie kupata kazi; hayo ni makosa makubwa. Unachopaswa kutafuta ni MAARIFA ili yakusaidie kupata kazi ya kufanya.
Wengi husema Pesa ni kila kitu katika dunia hii. Sio kweli lakini naweza kusema Pesa ina nafasi kubwa sana katika dunia lakini cha muhimu katika vyote hivyo ni MAARIFA maana naamini ukiwa na maarifa unaweza kuwa na chochote unachokitaka. Katika siku ya leo napenda tuangalie ni nini hasa nguvu ya maarifa na inakusaidiaje katika mambo yako.
VITABU ni nguvu kubwa sana ya maarifa ambayo inafanya watu wazidi kuwa wabunifu kila kukicha lakini changamoto kubwa ipo kwa Waafrika maana hadi siku umekuwepo msemo unaosema Ukitaka umfiche Mwaafrika kitu cha thamani Kiandike kwenye Kitabu
Mpendwa leo napenda kukuhamasisha tu ya kwamba ukitaka kufanikiwa na kuendelea kwa kasi ya 4g ni kusoma Vitabu maana katika vitabu unaweza kujizolea faida nyingi sana kama ifuatavyo;
Ubunifu watu wengi sana wamekuwa wabunifu na kuzidi kugundua mambo mapya sababu ya kusoma vitabu ambavyo vinawafanya kuwa welevu na kupata maarifa mbalimbali ambayo wanapoyatumia katika hisia chanya yanawaletea maendeleo makubwa sana katika maisha yao na jamii inayowazunguka.
Uhamasikaji ,Tupo kwenye dunia ambayo imejaa vikwazo na vigingi vingi sana watu wamekuwa wakikatishana tamaa sababu ya kukoswa maarifa ndugu ukiwa una nasoma vitabu utahamasika na kupata nguvu ya kufanya mambo makubwa ambayo hata ulikuwa hutarajii kufanya katika maisha yako.
Kutunza muda wako ndugu naamini unapokuwa unatenga muda wa kusoma vitabu itakufanya kuwa makini na muda wako na kujijengea tabia ya kujisomea, moja kwa moja unaanza kujijengea tabia ya kutunza muda. Hutapoteza tu muda na kuona huna cha kufanya kwa sababu muda wote una kitabu cha kusoma. Na pale ambapo una kitu cha kukusukuma umalize kitabu haraka kila dakika chache utakazopata utazitumia vizuri kusoma
Kuongeza Kipato chako Unapokuwa msomaji wa vitabu naamini utakuwa mbunifu , utahamasika ,utaweza kutunza muda wako kitu ambacho kitakuwezesha kuongeza kipato chako katika kitu chochote unachokifanya
Kuna faida nyingi sana unaweza kupata kupitia kusoma vitabu ndugu kama hujaanza au huna pa kuanzia naomba unitafute kwa namba na email iliyopo hapo chini niweze kukupa mwanga zaidi ni nini ufanye ili tuweze kwenda sawasawa na dunia yetu hii iliyojaa maarifa na ubunifu wa kila kukicha sio mwingine ni mimi muhamasishaji wako Yohana Shigukulu ahsante sana kwa muda wako kuutumia na kuweza kusoma makala hii naomba tukutane kwa makala zijazo.


1 comment:

  1. Moja ya silaha kubwa katika mafanikio ni kujua maarifa

    ReplyDelete