Sio swala la kushangaza mtu kumiliki pesa na kuishiwa pesa.
Unaweza kujiuliza kwanini watu wanapata pesa lakini kwa muda mfupi wanaishiwa?
Pesa imekuwa changamoto sana kwa watu wengi hadi imefikia hatua watu wanasema
pesa ni mashetani, mara wanasema pesa zina wenyewe. Jibu ni hapana Pesa sio
mashetani wala hazina wenyewe ila ni jinsi gani unakuwa na nidhamu punde
unavyokuwa na hiyo pesa.
Unaweza kujiuliza Nidhamu ya pesa ni nini? Nidhamu ya pesa
ni pale unapokuwa na uwezo wa kuicontrol pesa na kuweza kufanya kazi zako kwa
mipangilio bila ya kuja kujutia kwa badae. Mara nyingi sana watu wanashindwa
kujizuia pindi wanapokuwa na pesa sababu ya kukoswa nidhamu ya pesa.
Namna gani unaweza kuwa
na nidhamu ya pesa?
Ndugu, sizani kama hapo ulipo hujawahi kumiliki kiasi cha
pesa Fulani hapo nyuma. Hebu jaribu kuchukua hata muda wa dakika mbili ujiulize
hiyo pesa uliifanyia matumizi sawasawa na ambayo unafikiria ungefanya kama
ungekuwa nayo hiyo pesa.
Usijilaumu sana kwa matumizi hayo ya pesa yaweza kuwa labda
usingefanya hivyo usingefikia hapo ulipo haijalishi ni maisha mazuri au duni.
Sasa hebu tuangalie ni jinsi gani unaweza kuicontrol fedha na ukafanya vitu
ambavyo hutakuja kujutia baadaye.
Kwanza Jifunze kuweka bajeti. Wengi wetu tunapata pesa na
kuanza kufanya matumizi bila hata ya kubajeti pesa iliyopo sababu kubwa
inayopelekea watu wengi kutumia pesa hovyo mwisho wa siku baada ya pesa kuisha
ndio anakumbuka kufanya bajeti hewa yaani mtu anakumbuka kufanya mipango baada
ya pesa kumuishia.
Pili Panga manunuzi yako Kabla. Ni jambo la hekima na busara
kupangilia kile unachotakiwa kununua maana hili nalo limekuwa tatizo kubwa
linalowakumba watu mfano mtu anakwenda sokoni kununua nguo anafika huko anaongezea manunuzi
ambayo hata alikuwa hajapangilia halafu mwisho wa siku anaanza kujilaumu.
Tatu Tumia kidogo kuliko Unachokipata.Hapa ndio kuna shida
kubwa sana watu wanashindwa kusimamia mapato na matumizi na katika vitu viwili
ambavyo vinafanya mtu aendelee na asiendelee ni mapato na matumizi maana watu
wengi wanakuwa na matumizi ambayo yanazidi kipato kitu ambacho kinarudisha nyuma maendeleo.
Nne Jifunze kuweka rekodi ya matumizi yako. Kitu kinachoweza
kusaidia sana katika kuweka nidhamu ya pesa zako ni kurekodi ya matumizi
unayofanya hii itakusaidia kutathimini kiasi cha mapato na matumizi kwa muda
mwafaka na hivyo kukufanya utambue kama
unafanya maendeleo au laa.
Hizo ni baadhi ya njia zitakazo kufanya ujue nidhamu ya
pesa.hivyo unaweza kuona ni umuhimu gani unaoweza kuupata juu ya nidhamu ya
pesa .Katika siku ya leo napenda
nikwambie kitu kimoja. Pesa siyo kila kitu katika dunia hii lakini ina nafasi
kubwa sana. Hivyo ukitaka kuwa na utawala mzuri katika maisha yako ni vyema
ukaimarisha misingi ya matumizi ya pesa yako. Epuka tabia za kitoto au za watu
wasio kuwa na busara, ambao hula na kutumia kila wanachokipata Naamini njia
hizi zitakupa mwanzo mzuri wa matumizi ya pesa zako.

Pesa sio kila kitu katika dunia hii lakini ina nafasi kubwa sana.
ReplyDelete