Thursday, March 22, 2018

KIJANA NA HAMASA: SIRI KUBWA YA MAFANIKIO.


Ni siku nyingine tena tukiendelea na mfululizo wa makala hizi kwa undani zaidi siri ya kupata pesa (Utajiri) na kuendelea kuwa na pesa (Utajiri).
Watu wengi wamekuwa wakizunguka huku na huko wakitafuta hasa nini siri ya utajiri na wengine hadi kukimbilia imani potofu ili mradi tu wapate mali (Utajiri). Ni njia gani rahisi ambayo inaweza kuleta mafanikio kwa uharaka hili limekuwa ni swali ambalo linatawala vichwa vya wengi.
Na kitu kinachoponza zaidi ni pale mtu anapohitaji mafanikio kwa  urahisi na kwa haraka zaidi. Ndugu leo napenda nikupe siri moja tu ya mafanikio ambayo inaweza kuwa njia ya pekee ya kukuvusha daraja katika maisha yako.
Mafanikio hayatafutwi kwa dawa au zile imani potofu wanavyodai wengi. Mafanikio yanakuja pale mtu unapotambua anataka nini katika maisha yake. Maana yake kwanza anatakiwa atambue kwanini anataka utajiri au mafanikio? Halafu baada ya hapo akishapata sababu za kwanini anataka kuwa tajiri atafute sasa ni njia gani au namna jinsi afanye ili aweze kujikwamua sehemu alipo siyo kutafuta njia rahisi tu na ya haraka.
Watu wengi wamekuwa wakihoji na kuuliza kwa watu waliofanikiwa katika maisha yao kwamba ni njia gani wametumia hadi kufanikiwa? Jibu la moja kwa moja hapo ni kwamba huwezi ukajua ni njia gani zinazomfanya mtu afanikiwe kama hujajua kwanini unataka ufanikiwe katika maisha yako?. Maana mfano mzuri ni kwamba wengi husingizia tatizo ni mtaji lakini ni wangapi ambao wanakuwa na pesa za kuanzisha kitu chochote lakini anakaa muda mfupi tu anakuwa hana kila kitu kwahiyo ndugu kama hujajua kwanini unataka kuwa na mafanikio huwezi ukajua ni njia gani za kukufanya uwe na mafanikio.
Katika siku ya leo naomba uchukue tathimini dogo na ya haraka katika maisha yako Ni kweli katika maisha yako hujawahi kupata pesa ambayo kwa leo unafikiria ingekuwa mtaji kwako? Au Ni fursa ngapi umezipata hapo nyuma ambazo unafikiria ungekuwa nazo leo ungekuwa umejikwamua na maisha yako? Ndugu ukipata majibu ya maswali hayo naamini utakuwa umenielewa na kuelewa hasa nini siri kubwa ya mafanikio?
Sipo hapa kukukatisha tama maana unajua ni wapi ulipita lakini cha msingi hebu tafakari sasa kwa makini halafu ufanye yafuatayo;
1.       Acha kuendelea kuongea tu (Stop talking) najua una mipango mingi sana lakini cha kukushauri hebu acha kuishia kuwaza na kuongea tu na kuendelea  kupanga kila siku.
2.       Toa ndoto zisizo na kikomo (Stop dreaming) hizo ndoto ulizonazo haziwezi kutimia kwa kuwa nazo bila utekelezaji.
3.       Chukua hatua madhubuti ( Start Commiting) huu ni wakati wako kuanza kutekeleza kile unachokihitaji katika maisha yako acha woga mawazo yako ni sahihi hebu jaribu kutembea na hisia zako ili uweze kufanikiwa katika maisha yako.
Ndugu nashukuru sana kwa siku yako kuweza kufuatilia  huku nikiamini umenielewa na hili litakuwa ni chachu kubwa ya mafanikio yako ahsante sana kwa muda wako kwa siku ya leo naomba tukutane tena kwa makala zijazo ili tuendelee kujifunza zaidi kuhusu maisha yetu ni ukutakie uwe na siku njema

1 comment:

  1. hakika mafanikio yanakuja pale mtu anapoamua kuthubutu

    ReplyDelete