Koo za kuku
zinazopatikana hapa Tanzania; kuna koo nyingi za kuku zinazopatikana hapa
nchini;
Baadhi ya
koo hizo na sifa zake ni hizi
zifuatazo;-
1.
KUCHI
Sifa zake za kuchi;
a) Ana umbo lenye ukubwa wa wastani.
b) Hana upanga kichwani.
c) Ana mdomo mfupi.
d) Ana shingo ndefu yenye manyoya.
e) Ana ngozi ya rangi ya njano.
f) Ana miguu mirefu isiyo kuwa na
manyoya.
g) Ana uwezo mkubwa wa kujihami.
h) Wanapatikana mikoa ya Tabora ,
Singida , Shinyanga , Mwanza , na Tanga.
2.
KISHINGO
Sifa zake za kishingo;
a) Ana umbo lenye ukubwa wa wastani.
b) Ana upanga kichwani.
c) Ana shingo isiyo na manyoya.
d) Ana ngozi yenye rangi ya njano au
nyeusi.
e) Ana miguu mifupi isiyo kuwa na
manyoya.
f) Anapatikana mikoa yote Tanzania.
3.
BUKINI
Sifa zake za bukini;
a) Ana umbo fupi na ni mnene.
b) Ana upanga kichwani.
c) Ana shingo yenye manyoya.
d) Ana ngozi yenye rangi ya njano.
e) Hana manyoya ya mkia.
f) Wanapatikana kwa wingi katika mikoa
ya Tanga , Pwani , Kilimanjaro , na Singida.
g) Ana miguu mifupi isiyo kuwa na
manyoya.
4.
KINYAVU AU NUNGUNUNGU AU KUCHERE.
Sifa zake kinyavu;
a) Ana umbo dogo ukilinganisha na
kishingo na kuchi.
b) Ana shingo yenye manyoya.
c) Ana ngozi yenye rangi ya njano.
d) Ana manyoya yaliyosimama.
e) Ana mkia mrefu wa wastani.
f) Ana mkia mrefu wa wastani.
g) Anapatikana katika mikoa yote nchini.
5.
KAWAIDA UA KITEWE.
Sifa zake kitewe;
a) Ana umbo dogo ukilinganisha na kuchi
na kishingo.
b) Ana shingo yenye manyoya.
c) Ana ngozi yenye rangi nyeupe njano na
nyeus.
d) Ana manyoya ya mkia yenye urefu wa
wastani.
e) Anapatikana mikoa yote ya Tanzania.
Ndugu,
tambua unapofanya kitu ukiwa unakijua vizuri ni hakika utafanya kwa ufanisi zaidi ukilinganisha na
kama hujui. Ni fursa yako sasa kuchagua ni kuku wa aina gani unaweza kujikita
kufuga kwa maendeleo yako katika eneo ulilopo ahsante sana kwa leo naomba
tukutane kwenye makala ya LISHE YA KUKU
NA KUCHANGANYA CHAKULA.

0 comments: