Tuesday, October 9, 2018

AINA AU KOO ZA KUKU;




Koo za kuku zinazopatikana hapa Tanzania; kuna koo nyingi za kuku zinazopatikana hapa nchini;
Baadhi ya koo  hizo na sifa zake ni hizi zifuatazo;-
1.    KUCHI
Sifa zake za kuchi;
a)      Ana umbo lenye ukubwa wa wastani.
b)      Hana upanga kichwani.
c)      Ana mdomo mfupi.
d)      Ana shingo ndefu yenye manyoya.
e)      Ana ngozi ya rangi ya njano.
f)       Ana miguu mirefu isiyo kuwa na manyoya.
g)      Ana uwezo mkubwa wa kujihami.
h)      Wanapatikana mikoa ya Tabora , Singida , Shinyanga , Mwanza , na Tanga.
2.    KISHINGO
Sifa zake za kishingo;
a)      Ana umbo lenye ukubwa wa wastani.
b)      Ana upanga kichwani.
c)      Ana shingo isiyo na manyoya.
d)      Ana ngozi yenye rangi ya njano au nyeusi.
e)      Ana miguu mifupi isiyo kuwa na manyoya.
f)       Anapatikana mikoa yote Tanzania.
3.    BUKINI
Sifa zake za bukini;
a)      Ana umbo fupi na ni mnene.
b)      Ana upanga kichwani.
c)      Ana shingo yenye manyoya.
d)      Ana ngozi yenye rangi ya njano.
e)      Hana manyoya ya mkia.
f)       Wanapatikana kwa wingi katika mikoa ya Tanga , Pwani , Kilimanjaro , na Singida.
g)      Ana miguu mifupi isiyo kuwa na manyoya.
4.    KINYAVU AU NUNGUNUNGU AU KUCHERE.
Sifa zake kinyavu;
a)      Ana umbo dogo ukilinganisha na kishingo na kuchi.
b)      Ana shingo yenye manyoya.
c)      Ana ngozi yenye rangi ya njano.
d)      Ana manyoya yaliyosimama.
e)      Ana mkia mrefu wa wastani.
f)       Ana mkia mrefu wa wastani.
g)      Anapatikana katika mikoa yote nchini.
5.    KAWAIDA UA KITEWE.
Sifa zake kitewe;
a)      Ana umbo dogo ukilinganisha na kuchi na kishingo.
b)      Ana shingo yenye manyoya.
c)      Ana ngozi yenye rangi nyeupe njano na nyeus.
d)      Ana manyoya ya mkia yenye urefu wa wastani.
e)      Anapatikana mikoa yote ya Tanzania.
Ndugu, tambua unapofanya kitu ukiwa unakijua vizuri ni hakika  utafanya kwa ufanisi zaidi ukilinganisha na kama hujui. Ni fursa yako sasa kuchagua ni kuku wa aina gani unaweza kujikita kufuga kwa maendeleo yako katika eneo ulilopo ahsante sana kwa leo naomba tukutane kwenye makala ya LISHE YA KUKU NA KUCHANGANYA CHAKULA.

0 comments: