Nini maana
ya kustaafu?
Kustaafu
ni kuacha kazi kwa mujibu wa sheria , ama baada ya mkataba kuisha au kwa kuomba
kutokana na sababu mbalimbali kama za kiafya n.k
Kwa nini Ustaafu?
Kwa
haraka haraka mtu anaweza kujiuliza. Nini maana yangu ya kuandika kichwa cha
Kupanga kustaafu kama ninajua umeajiriwa au haujaajiriwa? Wengi wetu tunajua
neno kustaafu linatumika tu hasa kwa Watumishi wa Umma au Makampuni. Hapana
kustaafu anaweza kustaafu mtu yeyote kwenye kazi yake kutokana na sababu
mbalimbali. Na mimi siku ya leo napenda kukushauri upange kustaafu hebu twende
moja kwa moja ujue ni kwanini?
Nianze kwa kukuambia, Mwandishi wa kitabu cha Retire young
retire rich aliandika “Most people do not think about
retiring until its too late.” Kabla
sijaendelea naomba nikukumbushe makala ya nyuma nilitolea mfano wa safari ya
kwamba huwezi ukasafiri ukafikan hujui point yako ya mwisho (destination
point.) Wengi wetu tunajisahau sana kuhusu hili neno kustaafu tukitarajia hadi
tufikie uzeeni.
Kustaafu hakumanishi tu hadi uwe mzee au uajiriwe serikalini,
Je hufikirii kwa kazi hiyo uliyo nayo itafika muda ushindwe kufanya sawasawa na
leo? Au hujui kama fursa za leo si za kesho? Panga kustaafu, Si lazima ufikie
miaka 60 au zaidi ndio ufikirie kustaafu hebu angalia maisha yako ya kesho
yatakuwaje?
Ninapozungumzia kupanga kustaafu simanishi uache kazi
najaribu kukumbusha uwe na mipango ya kufanya kazi ambayo itakufanya ustaafu
mapema kwa maana ya kuwa na kazi ambayo itakuwa inakufanyia kazi siyo kuendelea
kufanya kazi hadi uzeeni.
Safari ya mafanikio ni kitendawili ambacho kimekuwa hakina
jibu la moja kwa moja na inapotokea unasafiri safari ambayo hujui utakuwa na
mapumziko ni sawa na kuwa mtumwa bila kujijua. Kuna vitu vingi unavyotakiwa
kufanya lakini hebu jaribu kuweka muda
wa kufikiria ni lini utapumzika katika safari yako hiyo?
Tupo vijana wengi tunaopata pesa na kuwa na matumizi ambayo hayafai
bila kufikiria kwamba nafasi tuliyo nayo leo hatujui kama itaendelea kuwepo
hadi kesho hali ambayo itakuja itugharimu katika uzee wetu na kubaki kulaani
bila sababu. Ndugu inawezekana kabisa kupata pesa na kuendelea kuwa na pesa
katika maisha yetu yote kama tutakuwa na mawazo chanya katika maisha yetu ya
kila siku
Kwa leo naomba tuishie hapa naomba tukutane tena kwa makala
zijazo kwa ajili ya kujifunza zaidi ni mimi muhamasishaji wako