Tupo kwenye
ulimwengu wa utandawazi, uliojaa maarifa ya kila aina , ulimwengu ambao upo
kwenye stage ya information age. Ni wazi kuwa mambo yamerahisishwa kila sekta,
watu tunaishi kama tupo kwenye kijiji kimoja. Mtu anapata mawasiliano na mtu
aliye mbali kwa muda mfupi tofauti na kipindi cha nyuma kitu ambacho kilikuwa
kinagharimu muda mrefu.
Kuna faida
nyingi sana za utandawazi tulio nao tukiutumia vizuri. Lakini naomba tukumbuke
penye faida , hasara hazikosekani. Hebu tuangalie ni nini hasa vijana wa leo
tumeathiriwa na utandawazi huu ambao kwa upande mwingine umetufanya kuwa
watumwa.
1.
Kila kitu kinawezekana (Everything is
possible).
Ni kweli kila kitu kinawezekana endapo tu jitihada binafsi zitatumika
lakini imekuwa ni viceversa kwa vijana wa sasa maana urithi mkubwa wa mafanikio
yao (muda) wanautumia vibaya na kuwa
na logic za tofauti na mafanikio yao lakini hawajui kwamba ‘’Thinking
success without struggling is as cooking an empty pot and waiting for soup.’’
2. Kutimiza ndoto ni kama kulala na
kuamka.
Maendeleo ni mabadiliko kutoka sehemu ya chini hadi juu (gradual
changes from low level to high level) kwa
maana ya mabadiliko ni kitu kinachochukua muda kwa maana ni kitu endelevu siyo
kitu cha kulala na kuamka. Sasa inapofikia stage hii vijana tulio wengi
tunachanganyikiwa na kuanza kuamini imani za tofauti ikiwemo kuamini utajiri
kutoka nguvu za ngiza hasa (free mason). Na kushindwa kuchukua maamuzi yaliyo
sahihi katika kufikia ndoto zetu.
Hakika katika vitu ambavyo hasa vijana hatujali ni muda yaani tunaona
kama swala la kawaida tu ambalo hata kesho tutakuwa hivyo hivyo. Lakini napenda
nikuambie mafanikio yangu na yako yanategemea sana muda tulio nao na tusije
tukafikiri muda huu tunaouchezea utakuja kujirudia tena




Its a nice app but there is no new updates,,,last posts ending 10 months ago,,how can we get new
ReplyDelete