Tuesday, March 13, 2018

KIJANA NA HAMASA: NGUVU YA MAWAZO YAKO.


Ndugu, Mpendwa ni tumaini langu wewe ni mzima wa afya tele. Itakuwa ni jambo njema ukichukua muda hata wa dakika moja uweze kumshukuru Mungu kwa hii nafasi uliyoipata siku ya leo. Maana kuna ambao walitamani kuiona siku hii lakini haikuwezekana.
Katika siku ya leo napenda nifungue ukurasa mpya ambao umekuwa ni changamoto kwa watu wengi sana wakiumiza vichwa ni namna gani ya kupata pesa(Utajiri) na kuendelea kuwa nayo siku zote.
Hebu tuweze kuangalia kwa undani ni namna gani NGUVU YA MAWAZO YAKO inaweza kukufanya upate pesa, halafu uendelee kukaa na pesa siku zote. Imefikia hatua hadi watu wanafanyiwa tunguli kwa sababu ya kulinda pesa zao lakini napenda nikuibie siri nzito sana leo.
Katika vitu vyenye nguvu na ambavyo vinafanya mtu afanikiwe ni uwezo wa akili yako (Power of your Mind), Tatizo linakuja pale Nguvu na Uwezo wa akili yako inapofanya kazi katika upande sahihi au usio sahihi. Mwandishi mmoja wa Kitabu aliandika (“One big difference between the rich and the poor is that poor people says “I can’t afford it;” more often than rich”) “Tofauti kubwa kati ya mtu tajiri na Mtu maskini ni Kwamba Maskini husema “Siwezi kufanya hiki” Tofauti na watu matajiri halafu akaendelea kusema (“Poor people use poor words and poor words create poor people means Your words do become flesh”) “Watu  maskini hutumia maneno ya kimaskini na maneno ya kimaskini hutengeneza watu maskini” na maneno yako waswahili wanasema Maneno huumba.
Katika ukurasa huu, ndugu naomba ujifunze tofauti ya maneno ya tajiri na maneno ya maskini , maneno yenye kasi kubwa na maneno yenye kasi ndogo na katika hili utatambua ni namna gani unaweza kubadilisha maisha yako kwa kutumia maneno yako na jinsi gani unavyofikiria na kama utaweza kubadili maneno yako na mawazo yako kama matajiri, ukawa na mawazo chanya  naamini ukipata pesa , utaendelea kuwa na pesa kwa urahisi sana
Ahsante sana kwa siku ya leo naomba tukutane kwenye makala ijayo .

0 comments: