Ndugu, mpendwa ni tumaini langu wewe ni mzima wa afya na
buheri tele. Ni jambo la kumshukuru Mungu. Maana ni vitu vingi tunavyokumbana
navyo ikiwa ni pamoja na kazi, majukumu, shida, matatizo, huzuni, starehe,
misukosuko na mambo mbalimbali kadha wa kadha.
Imekuwa desturi
na jambo la kawaida katika karne hii mtu kuwa na kazi nyingi(busy) na hata
kupelekea kukosa muda wa kupumzika na kuperuzi na vitu mbalimbali kwa ajili ya
kujitafutia riziki.
Ikiwa mimi na
wewe katika dunia hii ya utandawazi (Globalization) Dunia ambayo imejaa na
kuongezeka maarifa ni jukumu letu sote sisi kutafakari ni namna gani tunaweza
kuutendea muda wetu sawasawa na dunia inavyokwenda.
Napenda kutoa
shukrani zangu za dhati sana kwa kuchukua na kutoa muda wako kuweza kusoma na
kufuatilia ukurasa huu mpya wa “KIJANA NA
HAMASA”
Kijana ni nguzo kubwa na muhimu katika familia, ukoo, jamii
na hata taifa kwa ujumla. Kijana ni chombo kinachotegemewa sana katika maisha
ya mwanadamu ,maendeleo na shughuli zote zinazofanyika.
KWANINI KIJANA NA HAMASA?
Katika uhalisia
Nguzo ni kitu pekee kinachofanya kitu kionekane na hatimaye kiweze kutambulika
ni kitu gani? Kijana ni Uti wa Mgongo katika maendeleo na siku zote mafanikio
yanakuja pale mtu anapokuwa na hamasa ya maendeleo katika kazi, shughuli
anayofanya na kupelekea yeye kujitoa kifikra , mwili hadi kufikia pale
anapopahitaji.
KIJANA NA
HAMASA Ni ukurasa mpya wa blog unaoelezea na
kutoa ushauri mbalimbali ni jinsi gani na namna gani Vijana , Baba , Mama ,
Mzee unaweza Kujiwezesha na hatimaye Kufikia Malengo na kukamilisha ndoto zako
kwa muda sitahiki.
Fuatana name katika ukurasa huu ujue na utambue ni nini unatakiwa
kufanya katika karne hii ili uweze kufanikisha ndoto zako ikiwa ni faida kwako
, familia yako, ukoo wako , jamii inayokuzunguka na taifa kwa ujumla.
Ahsante sana kwa muda wako naamini utakuwa pamoja nami katika
makala zijazo ili tuweze kufanya kile kinachostahili kufanyika ili tuweze
kujenga maisha yetu na taifa kwa ujumla.
0 comments: