Friday, September 28, 2018

BADILI MATAZAMIO KUWA MALENGO


Imekuwa ni jambo la kawaida kila mwanzo wa kila mwaka watu kuwa na matazamio mbalimbali. Matazamio haya yamekuwa yakilenga hasa afya za watu, staili mbalimbali za maisha ikiwemo kupunguza uzito, kuacha kunywa pombe ,na kuvuta sigara, kupunguza matumizi ya pesa, na hata kufanya uwekezaji.
Lakini pamoja na hayo yote ,wiki chache tu zinapopita matazamio hayo husaulika hadi mwezi wa kumi na mbili unapokuja tena. Matazamio yamekuwa ni utangulizi wa kuweka alama kwa mwaka mpya tu. Katika makala hii hebu tujifunze na kluwa tofauti na ulenge hasa kwenye matazamio yako. Sasa ni namna gani unaenda kufanya matazamio yako kuwa malengo na klukufanya utimize ndoto zako.
Zifuatazo ni njia zitakazokufanya na kukusaidia uweze kufikia malengo yako ili utimize ndoto zako na siyo kubaki na ndoto zisizo timika.
1.     FANYA MATAZAMIO KUWA NDOTO ZAKO.
Watu wengi wamekuwa na utaratibu wa kuwa na matazamio na malengo halafu baada ya muda mfupi wanakata tamaa. Malengo yamekuwa na kufanywa ahadi za kawaida, ambazo zinakaa muda mfupi zinavunjika na kusahaulika. Ingawa kitendo cha kubadili matazamio hadi kuwa malengo ni kigumu sana na chenye kuhitaji kutumia akili nyingi hii yote ni kwa sababu Malengo na Ndoto ni kitu ambacho hupigania ili apate na kuondokana na shida alizonazo. Malengo ni kitu endelevu ambacho kinahitaji kukisimamia ili uweze kufikia ndoto zako.
2.     YAFANYE MATAZAMIO KUWA RAHISI.
Kosa la kwanza kabisa ambalo watu bwengi wanalifanya ni kuwa na malengo ambayo yanazidi maisha  yao na hii inapelekea kumfanya mtu aweze kukata tama haraka sana. Mabadiliko siku zote yanachukua muda na kutokana na hili mtu inakuwa ni vigumu sana kufikia malengo ambayo yanazidi kimo chake.
Kwamfano hauwezi ukawa na matazamio ya kuwa tajiri mkubwa duniani mwishoni mwa mwaka na wakati kwa sasa ni panya road. Na mvuta sigara vijiweni badala ya kuwa na mipangoya kuacha kuvuta sigara uanze mwanzo kama mtoto anayetembea kwa kuwa na matazamio kadri ya uwezo wako. Malengo yanapokuwa yamesetiwa makubwa kupita kiasi ni rahisi kufeli pindi mwili na akili zinapochukua muda mrefu kufanya kitu ambacho hakiwezekani . mabadiliko yanatakiwa kuwa taratibu na siyo harakaharaka.
3.     YAFANYE MATAZAMIO KUWA YA PEKEE.
Wakati unapopangilia mipango yako ya mwaka , ifanye mipango yako kuwa ya pekee. Upange mipango ambayo itakufanya ufikie mafanikio yako, mipango inayoainisha ndoto zako. Kama mtazamo wako ni kununua gari  sasa unatakiwa uainishe unataka kununua gari ya aina gani? Rangi yake na uweze kustick kwenye mipango yako ya kununua gari tu.
Watu mara nyingi huwa wana matazamio kwa mfanio aweze kupunguza uzito lakini anashindwa kuainisha kuainisha ni uzito wa kilo ngapi anatakiwa afikie . inakuwa ni vigumu sana kuona mabadiliko kitu ambachokitamfanya akate tamaa mapema.
4.     AINISHA MIPANGO YAKO.
Unaweza kuchora jedwali kwenye notebook la namna gani unaweza kufikia na kutimiza malengo yako. Kama malengo yako ni kutunza shillingi Millioni moja kwa mwaka sasa unatakiwa utengeneze bajeti ambayo kwa kila mwezi utakuwa unajaza kwenye jedwali lako na ukibainisha matumizi unayoyafanya. Au kwa mfano mtu ana mpango wa kuingia gym ni muhimu kubainisha ni gym gani unaenda kufanya, uitafute iko wapi, upange siku na muda sahihi wa kufanya gym.
5.     FURAHIA KIDOGO ULICHOPATA.
Watu hujifanya wagumu sana wanapokuwa pekee yao ukilinganisha wakiwa na watu wengine. Wanathubutu kujiadhibu wenyewe na kusababisha kushindwa kufikia malengo yao, maana unaposhindwa kutambua madogo uliyonayo utayatambuaje makubwa yale utakayoyapata?
Kusheherekea mafanikio hata kama yakiwa madogo ni muhimu sana kwa hatua ya mafanikio makubwa.
Kwa mfano unapokuwa na siku yako maalumu jaribu kuchukua muda hata wa lisaa limoja uweze kujipongeza mwenyewe kwa hatua uliyofikia  hata kama ni ndogo kiasi gani maana kupitia hicho kitu ulichokipata kitakupa hamasa na kukufanya uzidi kupiga hatua katika mafanikio yako.
6.     JIAMINI MWENYEWE.
Mwisho ,lakini muhimu sana ni jambo la kujiamini mwenyewe , hauwezi kufikia malengo yako kama  hauamini utayapata. Ni imani yako pekee itakayokufanya ufikie malengo yako. Inakuwa ni kitu cha ajabu mtu anapopanga kununua gari halafu hujiamini kama unaweza kununua,. Nguvu zote ambazo tunaanza nazo mwanzoni mwa mwaka tukijiamini na kwa ujasiri mkubwa hakika tutatimiza ndoto zetu.


0 comments: