Thursday, September 27, 2018

UFANYE NINI UPIGE HATUA KATIKA MAISHA YAKO?









UTANGULIZI.

Uchumi upo kwenye hali mbaya (Tatters), Kazi yako ipo hatarini (trouble) na kama una kazi yako hujui ufanye nini?
Ni takribani dunia nzima imekubwa na janga hili la uchumi na mara nyingi bila hata kupata ufumbuzi wa moja kwa moja lakini pamoja na hayo yote si swala la kuhoji ni namna gani na kwasababu gani hayo yote yamekuwa yakitokea ,Swala la msingi ni kwamba ni kwa namna gani tunaweza kuzitumia hizo taarifa na kuzifanya upande wetu kuwa ni jambo jema la kujivunia na kuweza kuleta maendeleo upande wetu.
Nimekuwa nikijifunza biashara na kazi mbalimbali kutoka kwa watu tofauti tofauti , wakiwemo watu mashuhuri walioendelea na ambao hawajaendelea , wasomi (veryn educated) na ambao hawajasoma lakini kwa namna moja au nyingine hao wotewamekuwa wakihangaika hangaika na kubaki kulaumu kuwa uchumi umekuwa ni mgumu sana.
Huwa nafikiria sana kwanini inatokea mtu maskini na mtu tajiri ingali wanaweza wakawa sehemu moja na wakifanya kazi moja. Kipindi nipo shule nilisoma sana kwa bidii zote nikitarajia kuwa huru katika maisha haya na kuamini kuwa Elimu pekee ndio msingi wa Maendeleo lakini kadri nilivyokuwa nikizidi kusoma mambo yalikuwa tofauti na matarajio yangu. Sikatai kuwa Elimu siyo msingi wa Maendeleo  ila unaitumiaje Elimu yako katika maendeleo yako.
Nimesoma vitabu mbalimbali vikiongelea juu ya maswala haya ya uchumi na kupata mwangaza wa kutosha na namna gani tunaweza kupata uzoefu kuweza kukabiliana na changamoto za uchumi. Na leo napenda nikusihi vitu vifuatavyo vya msingi katika makala hii ya “Timiza Ndoto”.
1.Tafakari una chagua kutimiza ndoto zako ili mwisho wa siku uweze kuwa huru kiuchumi wako au kuwa Mtumishi katika maisha yako.
2.Tafakari  juu ya utawala wako wa kifedha ikiwa unaitawala au inakutawala.
Nimekuwa nikijiuliza ni namna gani mtu anawezaje kupata utajiri (Wealth) na akaweza na kuweza kubakia na utajiri katika maisha yake yote na asiwe mtumwa tena katika utafutaji na kuweza kustarehe kabisa.
Ndugu kupitia ukurasa huu wa blog ya “Timiza ndoto” tutajifunza tufanye nini katika karne hii ya 21 ili tuweze kupiga hatua katika maisha yetu .lakini kabla hatujaanza kuangalia kwa undani ni namna gani tunaweza kupiga hatua katika maisha yetu napenda nikusihi kitu kimoja cha msingi sana ambachio katika mihangaiko yako ya kila siku panga kuwa na kazi yako ambayo inaweza kukuweka huru katika kufanya mambo unayoyataka katika maisha yako.
Ahsante sana kwa muda wako uliotumia napenda nikukaribishe katika mwendelezo wa kujifunza ni namna gani tunaweza kupiga hatua katika maisha yetu.

0 comments: