Kutokupatikana kwa ajira kunazidi kuongezeka. Je hufikirii kama nyakati zimebadilika. Nani anayejua? Hebu angalia nyuma uone ni jinsi gani ajira zilivyokuwa zinapatikana kwa urahisi halafu angalia na mfumo wa maisha ulivyo sasa hivi ujaribu kulinganisha. Tupo kwenye nguzo ya umeme tumenaswa na hatujui tufanye nini? Akili zetu zimefumbwa na hatuwezi kufanya chochote kama panzi waliotundikwa kwenye mti.
Uchumi sio
tatizo.tatizo ni nini? Najua una hasira pengine juu ya mambo ya siasa, rushwa,
serikali kutotimiza ahadi zake nzuri, kutokushughulikia haki za msingi za
binadamu au labda pengine una hasira wewe kama wewe kutotambua mapema.
Maisha ni
magumu sawa lakini swali la msingi unapata wapi suluhisho lake? Lawama na
miguno kukaa kujilaumu kwako kila siku hakuwezi kufanya kesho yako iwe vizuri
na kama unataka kesho yako iwe vizuri ni lazima uitengeneze leo na njia sahihi
ya kufanya ni kuwa na mtazamo chanya katika maisha yako ya baadaye ikiwa ni
pamoja na kuandaa mazingira ya kuwa na kazi yako.
Wengi
wanajiuliza “sasa ni kazi gani ya kufanya kwenye wakati mgumu huu wa uchumi?
“Huu ni wakati mzuri sana katika maana halisi ya neno ujasiriamali kwa maana ya
kwamba:,Ujasiriamali unahitaji kutatua changamoto ambazo ni ngumu na wakati
mgumu ikiwemo kubuni mbinu ambazo zitafanya mambo yawe rahisi. Unajua wengi
wanasema hali ni mbaya kwa sababu wanashindwa kutoa changamoto zao, lakini hebu
fikiria ukiwa kwenye shida, changamoto nyingi zimekubali huwa unafanya nini?
Pengine huwa unasolve mambo yako bila hata kujua ni njia gani umetumia.
Watu
wengi tumekuwa tukikimbilia ajira serikalini ili mradi tuwe na uhakika wa
maisha ya leo. Lakini vipi kuhusu kesho? Uhakika wa kula, kupata pesa hata
ukikwama kiafya, majanga mbalimbali yanapotokea kama ajali, vifo na vinginevyo
vimekuwa vikitazamwa sana na kusababisha watu kutafuta ajira serikali ili
waweze kujilinda na hayo. Na je inapotokea mtu anakoswa kazi anakuwaje? Hakika
tumekuwa na mentally disaster ambayo imelaza akili zetu na kushindwa kufikiri
ni namna gani tunaweza kuwa na kazi zetu ambazo zinaweza kutuweka financially
free.
Simanishi au
sisemi kama ajira ni kitu kibaya nayo pia ni njia mojawapo ya kujipatia kipato
na kumfanya mtu aweze kuishi vizuri. Maana tafasiri ya neno maendeleo kwenye
mind set za watu ni tofauti tofauti lakini tunapokuja kutaka kuwa huru katika
uchumi ni lazima tuwe na kazi zetu.

0 comments: