Monday, October 8, 2018

MAGONJWA YA KUKU





Magonjwa ya kuku:-
01.UGONJWA WA MDONDO
Ugonjwa huu huathiri kuku katika umri wowote na unapoingia kwenye kundi huweza kuua idadi kubwa ya kuku hao hadi kufikia asilimia tisini. Ndege wakubwa hustahimili kidogo kuliko wale wadogo kwa sababu ya usugu mwilini (body immunity) uliojengeka kwa muda mrefu zaidi.
       Ugonjwa huu husababishwa na kimelea cha kirusi kiitwacho Paramyxo viridae na huenezwa kwa njia ya  hewa na kugusana.
DALILI ZAKE.
·        - Kukohoa na kuhema kwa shida.
·         -Ute hutoka mdomoni na puani.
·       -  Kuku walioathirika hupata kizunguzungu.
·        - Kuharisha uharo wa kijani na njano.
·        - Kuzubaa, kusinzia na mabawa kushuka.
·         -Baada ya siku 2 kuku hupindisha shingo.
·         -Kuvimba macho.
·        - Kuku hutaga mayai hafifu.
·         -90% ya kuku huweza kufa.
TIBA.
Ugonjwa huu hauna dawa.
KINGA.
Chanja kuku wako kila baada ya miezi mitatu na mara nne kwa mwaka. Kuna chanjo za aina mbili za ugonjwa huu:-
                 1.  LASOTA
Chanjo hii hutolewa katika dawa yenye umbile la kidonge kimoja kimoja ambacho kina dozi ya kuku 1000 na huwekwa kwenye maji ili kuku wanywe hiyo dawa. Inashauriwa kuku wanaopewa dawa hii wanyimwe maji ya kunywa siku moja kabla yake.
Ni vizuri kuwapa mchanganyiko maalumu wa dawa wenye mchanganyiko wa vitamin na dawa ya kuwaongezea kuku nguvu. Dawa hii itolewe saa moja aui zaidi baada ya kuwapa chanjo ya mdondo.
2           2    THERMOSTABLE I2 NCD VACCINE.
Huwekwa katika chupa kimoja (vial) chenye dozi 400 za kuku. Chanjo hii inavumilia joto ikikaa bils nje ya jokofu kwa muda mrefu maana imetengenezwa katika mazingira ya nchi za joto na inaweza kukaa kwa siku 14-15 ikiwa itatunzwa ipasavyo hata baada ya kutumiwa mara ya kwanza.

02 KUHARISHA DAMU (COCCIDIOSIS).
Ugonjwa huu husababishwa na kimelea cha protozoa cha jamii ya Eimiria (Eimeria,tenela, Eimeria maxima na Eimeria accervunila).
Kwa kawaida  wadudu hawa hupenda kuishi kwenye mazingira machafu kama vinyesi, vyakula vilivyooza na umaji maji (Moist Environment).
DALILI ZAKE.
·        - Kinyesi chake huchanganyikana na damu.
·        - Wakati mwingine kuku hunya damu.
·         -Kuku hudhoofika sana.
·         -Kuku huteremsha mabawa yake.
·         -Hatimaye vifo hutokea.
TIBA
Ugonjwa huu hutibika kwa kutumia dawa za
                     i.            Kundi la sulphur:- mfano sulphonamides (ESB3) kwa siku 3-4.
                   ii.            Amprolium:- dawa za ugonjwa huu hupatikana madukani hivyo ukipatwa na tatizo hilo fika kwenye maduka ya dawa au muone mganga wa mifugo.
KINGA
-Zingatia usafi mara kwa mara kwa kuwa ugonjwa huu huambatana na maji maji na uchafu wenye vimelea vya ugonjwa huu , ni vizuri kuhakikisha banda la kuku linakuwa safi na wakati wote
-Tenga kuku wagonjwa kutoka kwa walio wazima  na tumia dawa ya kinga ili kuepudha uwezekano wa kuku kuambukizwa ugonjwa huu. Dawa inayopendekezwa ni zile zinazoitwa (coccidiostat)_ na  tenga kuku wadogo (vifaranga) kutoka kwenye kundi la wakubwa.

0 comments: